Search This Blog
Sunday, May 10, 2020
Mwakyembe "Ligi Kuchezwa Bila Mashabiki"
Serikali kupitia Waziri mwenye dhamana ya Michezo Dk Harrison Mwakyembe amesema wanaendelea kujadiliana na vyombo vinavyosimamia michezo nchini kuangalia jinsi watakavyoweza kurejesha michezo baada ya tamko la Rais Dk John Magufuli
Akizungumza baada ya kikao alichofanya na wadau, Dk Mwakyembe alisema ameliagiza Baraza la Michezo na Taifa (BMT) na TFF kuangalia jinsi wanavyoweza kuvisaidia vilabu kiuchumi ili kuweza kumudu gharama pale ligi itakaporejea.
“Tumewaagiza BMT na TFF wawasiliane na FIFA, CAF ili kuomba fedha za kusaidia vilabu wakati huu wa changamoto ya Corona”
“Ligi itakaporejea, kwa mechi kuchezwa bila ya mashabiki, timu zitakuwa kwenye wakati mgumu sana, Huu ni wakati ambao vilabu vinapaswa kusaidiwa na vyombo hivi ambavyo tunafahamu vina pesa ya kutosha,” amesema Dk Mwakyembe.
Tayari FIFA imetangaza kutoa mgawo wa zaidi ya Dola Milioni 150 kwa Wanachama wake katika jitihada za kuwasaidia kutimiza majukumu yao wakati huu wa kukabiliana na corona. TFF inatarajiwa kupokea zaidi shilingi bilioni moja kutoka mgawo huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment