Search This Blog
Sunday, May 3, 2020
Mchezaji wa Coastal Union Bakari Mwamnyeto kutua Simba SC
BAADA ya kuwepo kwa tetesi nyingi juu ya beki wa kati wa Coastal Union ya Tanga, Bakari Mwamnyeto kutakiwa na Simba, hatimaye uongozi wa Klabu ya Simba umeweka wazi juu ya suala hilo
Simba kupitia ofisi ya mtendaji mkuu wa klabu hiyo, Senzo Mazingisa inadaiwa kuwa imesema kuwa ni kweli mchezaji huyo inamuhitaji na tayari umeshampatia ofa yake ili aweze kujiunga na timu hiyo.
Akizungumza na mmoja wa viongozi wa Simba kutoka ndani ya ofisi hiyo ya Senzo alisema kuwa uongozi huo upo tayari kutoa kitita cha Sh milioni 80 ili kumsajili mchezaji huyo.
Mtoa taarifa huyo ameeleza kuwa Sh milioni 50 ni kwa ajili ya Mwamnyeto mwenyewe na Sh milioni 30 ni kwa ajili klabu yake ya Costal Unioni kama ada ya uhamisho wake kwa kuwa bado ana mkataba.
“Ofa hiyo tulimpatia tangu dirisha dogo la usajili lakini akaikataa kuwa ni kidogo anataka yeye peke yake achukue Sh milioni 80 zote.
“Jambo hilo uongozi haukukubaliana nalo na ukaamua kuliacha kama lilivyo, kwa hiyo kama atakubali kuchukua kiasi hicho basi atasajiliwa kama hakikataa basi akatafute timu nyingine,” kilisema chanzo hicho cha habari.
Alipotafutwa Senzo ili azungumzie hilo hakupatikana lakini kwa upande wake, Mwamnyeto yeye hakutaka kusema chochote kuhusiana na hilo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment