Machafuko yanaripotiwa kuongezeka katika mkoa wa Ituri katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuzidi kuzusha wasiwasi miongoni mwa raia wa mkoa huo.
Taarifa zaidi zinasema kuwa, mashambulio kadhaa yameripotiwa katika maeneo 4 kati ya 5 ya mkoa wa Ituri, kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya KIdemokrasia ya Congo.
Wiki hii, Wabunge na Maseneta kutoka mkoa wa Ituri walikutana na Jeanine Mabunda na Alexis Thambwe Mwamba, Maspika wa Bunge la Kitaifa na Bunge la Seneti, ili kuomba hatua zaidi kutoka kwa mamlaka zichukuliwe dhidi ya makundi yanayohusika na machafuko hayo katika maeneo hayo.
Mwezi uliopita Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa (OHCHR) ilisema katika ripoti yake kuwa, zaidi ya watu 150 wameuawa katika mkoa wa Ituri katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika kipindi cha siku 40 zilizopita.
Mamia ya Wakongomani wameuawa katika mashambulizi ya wanamgambo wa ADF-Nalu ambao asili yao ni Uganda hususan katika maeneo ya mashariki mwa nchi, tokeo mwaka 2014.
Wiki iliyopita, wanamgambo 23 waliuawa katika mapigano baina yao na Jeshi la Ulinzi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC) katika mkoa wa Ituri, kaskazini mwa nchi.
Eneo la mashariki mwa DRC limekuwa likishuhudia machafuko ya mara kwa mara baina ya makundi ya wanamgambo kwa upande mmoja na wanamgambo na maafisa usalama kwa upande mwingine, kutokana na kuwa na utajiri mkubwa wa madini hususan dhahabu na almasi.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment