Search This Blog
Wednesday, May 27, 2020
Idadi ya wagonjwa wa corona Zanzibar yapungua, 115 wamepona
Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi amesema hadi kufikia leo mei 27,2020 kuna jumla ya watu 134 wamethibithibitishwa kuumwa Corona Zanzibar, 115 wamepona na 19 bado wanaendelea na matibabu.
Akizungumza kwenye televisheni ya Taifa ya Zanzibar (ZBC) leo amesema kupungua kwa wagonjwa kumetokaana na kufuata maagizo ya viongozi wa juu wa kitaifa.
“Jumla ya wagonjwa 115 wamepona ugonjwa huu na mpaka sasa wamebakiwa wagonjwa 19 tu wanaopatiwa matibabu kwenye vituo vya kutibu wagonjwa hawa nchi nzima ” amesema Balozi Iddi.
Ikumbukwe kuwa mgonjwa wa kwanza wa Corona Zanzibar aligunduliwa mnamo mwezi Machi na tangu hapo kumekuwa na kambi maalum za kutibu wagonjwa wa corona visiwani humo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment