Search This Blog
Wednesday, May 27, 2020
Idadi ya vifo vya corona yafikia 100,276 Marekani
Idadi ya wagonjwa waliofariki kutokana na virusi vya corona nchini Marekani imepita 100,000 katika kipindi cha chini ya miezi minne.
Taifa hilo limeandikisha vifo vingi zaidi ya taifa lolote lile huku watu milioni 1.69 wakithibitishwa kuambukizwa virusi hivyo idadi ambayo ni asilimia 30 ya maambukizi yote duniani.
Maambukizi ya kwanza nchini Marekani yaliripotiwa mjini Washington tarehe 21 mwezi Januari.
Kote duiniani kumekuwa na watu milioni 5.6 walioambukizwa virusi hivyo huku idadi ya vifo ikifikia 354,983 tangu mlipuko wa virusi hivyo kuzuka mjini Wuhan nchini China mwisho wa mwaka jana.
Kufikia sasa idadi ya waliofariki nchini Marekani imefikia 100,276, kulingana na Chuo kikuu cha John Hopkins mjini Maryland ,ambacho kimekuwa kikifuatilia mlipuko huo.
Muhariri wa BBC katika eneo la Marekani ya kaskazini Jon Sopel anasema akwamba idadi hiyo ni sawa na idadi ya wanajeshi wa Marekani waliouawa katika vita vya Korea, Vitenam, Iraq na Afghanistan katika kipindi cha miaka 44 wakipigana.
Hatahivyo Marekani imeoredheshwa ya tisa duniani kwa kiwango cha watu wanaofariki nyuma ya Ubelgiji, Uingereza , Ufaransa na Ireland kulingana na chuo hicho.
Jimbo la North Carolina , Wisconsin na Arkansas ni miongoni mwa yale yanayoandikisha ongezeko la wagonjwa wanaofariki.
Hatahivyo idadi ya wanaofariki inaendelea kuongezeka katika miji mikuu ikiwemo Chicago, Los Angeles na makaazi ya Washingtin DC.
Hatahivyo idadi ya wanaofariki katika majimbo yalioathirika zaidi imeanza kupungua ikiwemo New York ambapo watu 21,000 wamefariki.
Wakati wa kilele cha maambukizi hayo katika mji huo, idadi ya vifo vya kila siku ilikuwa mamia.
Hospitali ziishindwa kuhimili idadi hiyo huku vyumba vya kuhifadhi maiti kwa muda mfupi vikijengwa nje ya hospitali hizo.
Je janga hilo limekabiliwa vipi kisiasa?
Rais Donald Trump amesisitiza kwamba iwapo utawala wake usingechukua hatua yoyote idadi ya vifo ingekuwa mara 25 zaidi ya ilivyo sasa ijapokuwa wakosoaji wake wamemkosoa kwa kuchelewa kuchukua hatua.
Magavana pia wamelaumumiwa kwa kutochukua tahadhari za mapema kwa tisho la virusi hivyo katika nyumba za wazee.
Awali , rais huyo wa chama cha Republican alipuuza mlipuko huo akiufananisha na mlipuko wa homa ya msimu.
Mapema mwezi Februari alisema kwamba Marekani imedhibiti virusi hivyo na kwamba ifikiapo mwezi Aprili vitakuwa vimeisha.
Alitabiri kwamba kutakuwa na vifo 50,000-60,000 kabla ya ugonjwa huo kudhibitiwa kabisa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment