Search This Blog

Saturday, May 16, 2020

Hotuba ya Upinzani yakataliwa kusomwa Bungeni,Spika atoa sababu

Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai, ameikataa Hotuba ya Wizara ya Fedha kutoka Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, kwa kile alichokidai kuwa hotuba hiyo imeandaliwa na Mbunge ambaye hayupo ndani ya Bunge hilo.
Kupitia vikao vya Bunge ambavyo ameviendesha leo Mei 15, 2020, Bungeni jijini Dodoma Spika Ndugai ameendelea kusema kuwa, hajaikubali hotuba hiyo kwa kuwa mwandishi wa hotuba hiyo ni Mbunge Halima Mdee na hayupo ndani ya Bunge.
"Hotuba ya kambi rasmi hatujaikubali sababu mwandishi wake ni Halima Mdee ni kati ya wale waliojifukuza wenyewe Bungeni, kwamba roho zao ni muhimu kuliko wengine, haiwezekani ukapitishia dirishani kazi zako zikafanyika, wakati wewe hata uliko hakujulikani" amesema Spika Ndugai


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...