Kupitia vikao vya Bunge ambavyo ameviendesha leo Mei 15, 2020, Bungeni jijini Dodoma Spika Ndugai ameendelea kusema kuwa, hajaikubali hotuba hiyo kwa kuwa mwandishi wa hotuba hiyo ni Mbunge Halima Mdee na hayupo ndani ya Bunge.
"Hotuba ya kambi rasmi hatujaikubali sababu mwandishi wake ni Halima Mdee ni kati ya wale waliojifukuza wenyewe Bungeni, kwamba roho zao ni muhimu kuliko wengine, haiwezekani ukapitishia dirishani kazi zako zikafanyika, wakati wewe hata uliko hakujulikani" amesema Spika Ndugai

No comments:
Post a Comment