Search This Blog

Tuesday, May 12, 2020

BOT kupunguza riba ya mikopo

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Florens Luoga amesema kuwa Kamati ya Sera ya Fedha ya Bodi ya Benki Kuu ya Tanzania iliyokutana Mei 8 mwaka huu imepitisha hatua mbalimbali za kisera zinazolenga kukabiliana na athari za mlipuko wa Ugonjwa wa homa ya virusi vya Corona COVID-19 katika Uchumi lengo la hatua hizo likiwa kudumisha udhibiti wa sekta ya fedha na upatikanaji wa huduma za fedha kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Gavana Luoga amesema Kamati hiyo katika sera hizo imekubaliana Benki kushusha kiwango cha chini cha kisheria cha sehemu ya Amana kinachotakiwa kuwekwa Benki Kuu ya Tanzania kutoka asilimia 7 hadi 6 kuanzia Juni 8 mwaka huu huku ikitarajiwa kuongeza ukwasi katika Sekta ya Benki.

Aidha Benki Kuu kushusha kiwango cha riba kinachotozwa kwa benki kukopa benki kuu kutoka asilimia 7 hadi asilimia 5 kuanzia Mei 12 mwaka huu hatua itakayowezesha kuongeza wigo wa benki kukopa kutoka Benki Kuu kwa riba nafuu na hivyo kupunguza riba ya mikopo kwa wateja.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...