Vifo kutokana na janga la virusi vya corona katika mataifa ya Ulaya yaliyoathirika kwa kiasi kikubwa vimefikia zaidi ya laki moja hadi kufikia jana, wakati nchini Marekani mamia ya waandamanaji wakitiwa nguvu na rais Donald Trump waliandamana dhidi ya amri ya kutotoka nje inayoathiri uchumi wa nchi hiyo.
Wasanii kutoka sehemu mbali mbali duniani walifanya tamasha la muziki lenye nia ya kuwaunga mkono wafanyakazi wa sekta ya afya , na kuleta hali ya umoja wa kijamii katika wakati huu wa mzozo.
Tukio hilo lililochukua muda wa masaa sita mtandaoni lilijumuisha waimbaji kama Billie Eilish na Rolling Stones, lililotayarishwa na kundi la utetezi la Global Citizen pamoja na shirika la afya ulimwenguni WHO.
Duniani kiasi watu 2,281,334 wamepatikana na maambukizi ya virusi vya corona hadi sasa.
Mataifa ya Ulaya yamekabiliwa na vifo vya watu 100,510 , ikiwa karibu theluthi mbili ya watu wote 157,163 waliofariki duniani kote, kwa mujibu wa idadi iliyotolewa na shirika la habari la Ufaransa AFP, wakati karibu robo ya vifo vimetokea nchini Marekani.
Watu 38,000 wamefariki nchini Marekani hadi jana Jumamosi, kwa mujibu wa idadi iliyotolewa na chuo kikuu cha Johns Hopkins.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment