Search This Blog

Saturday, April 11, 2020

Uturuki yatuma msaada wa vifaa vya matibabu nchini Uingereza

Uturuki yatuma msaada wa madawa na vifaa vya matibabu nchini Uingereza katika juhudi za kupambana na virusi vya corona.

Uturuki yafahamisha kutuma msaada wa madawa na vifaa vyamatibabu nchini Uingereza katika uhudi za kupambana na virusi vya corona, virusi ambavyo tayari vimesababisha maafa makubwa ulimwenguni.

Ndege ya mizigo ya  jeshi imeondoka mapema Ijumaa katika uwanja wa ndege mjini Ankara kuelekea nchini Uingereza.

Msaada huo ni pamoja na  barakoa  aina ya N95 na  vifaa vingine ambavyo hutumiwa katika  kuzuia maambukizi  ya Covid-19.

Wizara ya afya ya Uturuki imesema kuwa kuwa vifaa  hivyo ni kwa ajili ya ushirikiano katika kupambana  dhidi ya virusi vya corona.

Ndege hiyo aina ya A400M anasubiriwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa  mjini London.

Katika  mikoba ya vifaa hivyo kumechapishwa  beti za shairi şa Mevlana Jalal ad Din Rumi zisemazo : «  kuna matumaini  hata kama watu wamepoteza matumaini".

Uturuki imetuma pia msaada wa  madawa na vifaa vya matibabu nchini Italia, Uhispania, Mekedonia Kaskazini, Montenegro, Serbia, Boznia na Kosovo.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...