Search This Blog
Thursday, April 2, 2020
Simba walikua na haki ya kunifuata - Morrison
Kiungo mshambuliaji wa Yanga Bernard Morrison, amesema kuwa Simba walikuwa wana uhuru wa kuzungumza naye ili kumpa dili kwa kuwa yeye ni mchezaji mzuri na anajua uwezo wake alionao habahatishi.
Kiungo huyo mwenye mabao matatu alikuwa anawindwa na wapinzani wa Yanga ambapo walitaka kuipata saini yake jambo lililokwama mwishoni baada ya Yanga kumpa dili la miaka miwili.
Morrison amesema kuwa ilikuwa ni rahisi kwake kuingia kwenye akili za Simba kwa kuwa ni mchezaji mzuri na wao wana haki ya kufanya hivyo.
"Ilikuwa ni haki yao kunifuata na kuzungumza nami ili kupata saini yangu kwa kuwa mimi ni mchezaji mzuri na ninaipenda kazi yangu.
"Walinifuata kabla ya mechi yetu dhidi ya Yanga ambapo tulishinda na kupata pointi tatu, nililiacha suala hilo mikononi mwa wakala wangu," amesema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment