Search This Blog

Wednesday, April 22, 2020

Msanii JayDee Asema Corona sio Ugonjwa wa Kuficha ni Vizuri Wakaweka Wazi



Msanii wa Muziki wa Bongo Flave, Judith Wambura maarufu kwa jina la Lady JayDee amesema Corona si kitu cha aibu mtu akipata ifichwe.

“Sio ugonjwa wa zinaa useme aliyeupata alizini kwa hiyo iwe siri kumsitiri. Hii ni ya wote,” aliandika ujumbe huo katika ukurasa wake wa Twitter.

Msanii huyo amesema kuweka wazi kunaweza kusaidia watu kuwa makini zaidi “Mtazamo tu si lazima niwe sahihi. #staysafe,”.

” Corona si kitu cha aibu mtu akipata ifichwe, sio ugonjwa wa zinaa useme aliyeupata alizini kwa hiyo iwe siri kumsitiri. Hii ni ya wote, kuweka wazi kunaweza hata kusaidia watu kuchukulia serious na kujilinda zaidi. Mtazamo tu si lazima niwe sahihi. #staysafe,”.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...