Mamia ya watu walishiriki maandamano jana katika miji ya Berlin na Stuttgart nchini Ujerumani kupinga hatua zilizowekwa na serikali kuilinda nchi dhidi ya virusi vya corona.
Karibu waandamanaji 1,000 walikusanyika katika mji mkuu wa Ujerumani wakisema kwa sauti kubwa "Ninataka kurudishiwa maisha yangu" na kubeba mabango yenye ujumbe kama vile "Zilinde haki za kikatiba".
Waandamanaji walisambaza magazeti yanayohoji umuhimu wa hatua za kuwafungia watu majumbani na kudai kuwa virusi vya corona ni jaribio la kunyakua madaraka kwa kueneza hofu.
Ilikuwa ni Jumamosi ya nne mfululizo ya maandamano mjini Berlin.
Mjini Stuttgart, kati ya watu 350 na 500 waliingia mitaani huku kiongozi wao akisema maandamano hayo yalikuwa ya kuunga mkono haki za msingi kama vile uhuru wa kukusanyika na uhuru wa kuabudu.
Mkusanyiko huo ulikuwa umepigwa marufuku kabla ya kuruhusiwa na Mahakama ya Kikatiba.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment