Search This Blog

Sunday, April 26, 2020

G20 yazindua mpango wa vifaa vya kiafya kupambana na corona

Kundi la nchi 20 tajiri na zinazoinukia kiuchumi duniani - G20 zimezindua leo mpango wa kimataifa wa kuharakisha upatikanaji wa vifaa vya kiafya vinavyohitajika kupambana na virusi vya corona.

Waziri wa fedha wa Saudi Arabia, ambayo ni mwenyekiti wa sasa wa G20, Mohammed al-Jadaan amesema kundi hilo bado linajitahidi kuziba pengo la ufadhili wa takribani dola bilioni 8 wa kupambana na janga hilo.

Ameongeza kuwa jamii ya kimataifa bado inakabiliwa na hali ya kutokuwa na uhakika kuhusu ukubwa na muda ambao janga hili la kiafya litatatuliwa.

Saudi Arabia mapema mwezi juu iliahidi dola milioni 500 za kuunga mkono juhudi za kimataifa za kupambana na janga la virisi vya corona.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...