Search This Blog
Tuesday, April 21, 2020
Kinachoendelea kuhusu kifo cha mama Rwakatare
Familia ya Askofu Dr. Gertrude Rwakatare, imesema kuwa kwa sasa bado inasubiri taratibu za kikao cha familia pamoja na Serikali kabla ya kutoa taarifa kuhusu msiba huo.
Mtoto wa marehemu ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kawe Mkoani Dar es salaam, Bw. Muta Lwakatare, amewaasa wapendwa wa marehemu mama yake kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho taratibu zinasubiriwa.
Amesema kuwa watu wanaweza kufika nyumbani kwa marehemu kwa ajili ya kutoa pole, lakini ni kwa utaratibu maalum wa kuepuka mikusanyiko ikiwa ni hatua za kukabiliana na ugonjwa wa virusi vya Corona.
Hatua hiyo inakuja ikiwa ni siku moja imepita tangu kifo cha Mchungaji na Askofu wa Kanisa la Mlima wa Moto, Dr. Gertrude Rwakatare kilichotokea Alfajiri ya jana Aprili 20, katika Hosptali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam, alikokuwa akipatiwa matibabu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment