Staa wa muziki nchini, Harmonize amefunguka na kusema yuko mbioni kuachia wimbo wa taarab na atamshirikisha Mzee Yusuph pindi atakaporudi mjini.
Hivi karibuni aliyekuwa Mwimbaji nguli wa muziki wa Taarab nchini, Mfalme Mzee Yusuph aliweka wazi anatarajia kurejea kwenye muziki ila watu wangoje ni kitu gani hasa atakuja kuimba.
Harmonize akiwa kwenye kipindi cha Uhondo, E FM Radio aliimba kionjo cha wimbo huo ambao kwa sasa anauandaa.
Itakumbukwa, Mzee Yusuph ana miaka takribani 6 tangu alipotangaza kuachana na muziki huo na kuanza kuimba Qaswida zenye maudhui ya dini ya kiislam. Je akirudi mjini atakuja na maadhi gani ya muziki? Mimi na wewe hatujui, tufanye kusubiri.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...
No comments:
Post a Comment