Kwenye mahojiano ya njia ya simu na kipindi cha "Rick and Sasha", Braxton alitoa taarifa hiyo ambapo alisema licha ya kupitia changamoto nyingi yeye na mchumba wake #Birdman katika maisha yao, hatimaye watafunga ndoa na wamepanga kutofanya harusi kubwa.
Katika kusisitiza ni lini harusi hiyo itafanyika, #Braxton (52) alisema.. "Tumejaribu kupanga, lakini kwa uhakika tutafunga ndoa mwaka huu" alisema Braxton.
Itakumbukwa, wawili hao walianza mahusiano Mei 2016 na kutangaza uchumba wao Februari 2018. Januari 2019 walitangaza kuvunjika kwa uchumba wao, baadaye April 2019 walitangaza tena kuwa bado wapo pamoja.

No comments:
Post a Comment