Search This Blog

Sunday, March 8, 2020

Uturuki yawaokoa wahamiaji 121 katika bahari ya Egean


Kikosi cha kulinda pwani cha Uturuki chawaokoa wahamiaji 121 katika bahari ya Egean.

Mzozo wa wahamiaji na wakimbizi  mpakani mwa Uturuki na Ugiriki,  kikosi cha kulinda pwani cha jeshi la Uturuki chafahamisha kuwaokoa wahamiaji na wakimbizi 121 katika bahari ya Egean.

Wahamiaji waliokwama majini  waliotoa ishara ya kuomba msaada na kikosi hicho  kutoa msaada katika bahari ya Egean walipokuwa wamekwama.

Wahamiaji hao walikwama walipokuwa katika boti katika   mbali ya mita kadhaa na ardhi ya Çeşme mkoani Izmir upande wa  Magharibi.

Mwanahabari wa shirika la Anadolu amefahamisha kwamba wakimbizi waliookolewa walikuwa wakielekea katika visiwa vya  Ugiriki vinavyopatikana katika bahari ya Egean.

Taarifa nyingine imefahamisha kuwa  maboti mengine  yaliokolewa yalikuwa na  raia wa Afghanistani 47, Syria 49 na 24 kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo mkoani Izmir.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...