Search This Blog

Sunday, March 8, 2020

Rais wa Uturuki: Hatutosita kaunza upya operesheni iwapo jeshi la Assad litakiuka makubaliano


Rais wa Uturuki azungumza kuhusu makubaliano ya kusitishwa mapigano Idlib na kusema kuwa jeshi lipo tayari iwapo makubaliano yatakiukwa.

Rais wa Uturuki Recep Tayyıp Erdoğan asema kwamba jeshi la Uturuki halitosita kuanza upya operesheni yake iwapoa jeshi la Assad litakiuka makubaliano Idlib.

Kwa mara nyingine rais Erdoğan amekumbusha kuwa kamwe Uturuki haina lengo la kuhujumu ardhi ya Syria katika operesheni zake.

Kwa mujibu wa rais Erdoğan watoto na wanawake ndio waathirika waliomstari wa kwanza katika mapigano yanayoendelea nchini Syria.

Rais Erdoğan amesema kuwa ameshangazwa kwa kutoona yeyote anaekemea madhila yanayowakumba watoto na wanawake katika vita na mauji  ya Syria.

Hayo rais Erdoğan ameyazungumza katika hotuba yake aliotoa katika  hafla ilioandaliwa katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wanawake.

Siku kuu hiyo nchini Uturuki imeandaliwa kwa kuwaenzi wanawake waliojitolea kulilinda  taifa la Uturuki.

Hakuna yeyote aliezungumza  kuhusu wanawake wanaotaabika miongoni mwa wahamiaji  zaidi ya  100 000 wanaonyanyaswa wanaotaka  kwenda katika mataifa ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...