Search This Blog

Tuesday, March 17, 2020

Umeme wa TANESCO kushusha bei


Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu amesema kuwa bei ya umeme itashuka baada ya kukamilika kwa ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa Julius Nyerere kutokana na gharama nafuu ya uzalishaji umeme kwa maji kuwa nafuu (Shilingi 36 kwa yuniti) ukilinganisha na vyanzo vingine mfano gesi ambayo hugharimu Shilingi 147 kwa yuniti moja.

“Baada ya punguzo la bei ya umeme tunatarajia hata viwandani gharama za uendeshaji zitashuka na hivyo mabadiliko hayo yatakwenda sambamba na kupungua kwa bei ya mali na bidhaa mbalimbali zinazozalishwa viwandani hapa nchini hivyo kupunguza mfumoko wa bei na kuviwezesha viwanda vyetu kufanya ushindani kimataifa” amesema Naibu Waziri Subira Mgalu

Kwa upande wake Arun Lodhia, ambaye ni mmiliki wa kiwanda cha Lodhia Group kinachozalisha bidhaa za chuma na plastiki amesema, kiwanda chake kinatarajia kupata ahueni kubwa endapo bei ya umeme itapungua na wataweza kushusha bei ya bidhaa zao.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...