
MANCHESTER, ENGLAND . REAL Madrid na Barcelona zimeingia kwenye vita ya kuisaka saini ya winga wa Manchester City, Leroy Sane, anayefukuziwa na Bayern Munich.
Bayern ilikaribia kumnasa Sane wakati wa kiangazi mwaka jana, lakini majeraha ya goti yakasababisha abaki Man City, huku miamba hiyo ya Ujerumani ikimfuatilia kwa karibu.
Tayari kuna taarifa Mkurugenzi wa Michezo wa Bayern, Hasan Salihamidzic amekutana na wakala wa mchezaji huyo kuona uwezekano wa kumsajili wakati wa kiangazi.
Lakini, sasa Bayern itajikuta kwenye vita kali ya kuwania saini ya winga huyo baada ya Madrid na Barcelona kuingia kwenye harakati za kuisaka saini ya Mjerumani huyo.
No comments:
Post a Comment