Search This Blog

Saturday, March 28, 2020

Kwa Manyika kila kitu freshi

By Olipa Assa

KIPA wa Polisi Tanzania, Peter Manyika  Jr amesema licha ya kusimama kwa ligi kutokana na kuepuka maambukizi ya ugonjwa wa corona, anapata msaada wa baba yake mzazi unaomsaidia kulinda kiwango.
Baba wa mchezaji huyo, Manyika Peter Sr ni kocha wa makipa wa timu ya Yanga,amekuwa akimpa mazoezi mwanae kuhakikisha kiwango chake hakishuki.
Manyika Jr ameliambia Mwanaspoti kwamba baba yake anamsimamia mazoezi na kumshauri namna ya kukuza kiwango chake.
"Msaada wa baba umekuwa mkubwa,licha ya kunisimamia kwa baadhi ya mazoezi bado kuna programu alizonipa zakufanya binafsi,"
"Nimebahatika kuwa na baba ambaye anafuatilia hatua zangu moja baada ya nyingine kuhakikisha sirudi nyuma kwenye kazi zangu,"amesema.
Tangu ajiunge na timu hiyo  akitokea nchini Kenya ambako alikuwa anacheza klabu ya KCB, amedaka mechi tatu dhidi ya Singida United, Ndanda na Mwadui ambapo aliweza kuokoa hatari mbili.

Let's block ads! (Why?)

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...