Search This Blog

Sunday, March 22, 2020

Hispania: Virusi vya corona vyaongezeka kwa asilimia 30 kwa siku

Uhispania jana imetangaza vifo vipya 394 vilivyosababishwa na virusi vya corona, na kufanya jumla ya vifo vilivyotokea nchini humo kufikia 1,720.

Idadi hiyo inalalifanya taifa hilo kuwa la pili kwa idadi ya vifo, baada ya Italia. Idadi hiyo ni sawa na ongezeko la asilimia 30 ikilinagnishwa na siku moja iliyopita.

Na idadi ya waliothibitishwa kuwa na virusi imeongezeka kutoka watu 3,646, sawa na asilimia 14.6, hadi watu 28,572.

Wizara ya afya ya Uhispania imeonya kwamba maambukizi yataongezeka zaidi kwa siku zijazo.

Upo wasiwasi wa kuwepo kwa mrundikano wa watu katika hospitali nyingi nchini humo katika wakati huu ambao watu walio katika uangalizi wa wagonjwa mahututi ikifikia 1,785.

Hapo jana Waziri Mkuu wa Uhisapania Pedro Sanchez alisema mripuko huo ni kati ya hali mbaya zaidi ulimwenguni, na itaendelea kuzorota zaidi.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...