Search This Blog

Friday, March 27, 2020

Gambo "Lema Hupewa VIBALI vya Mikutano wa Hadhara Lakini Ameacha Kwa Kukosa Watu"

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema Mbunge wa Chadema katika jimbo la Arusha mjini Godbless Lema hupewa kibari cha kufanya mikutano ya hadhara kila anapoomba mpaka anaacha kufanya mwenyewe.

“Mikutano yote aliyoomba Mbunge Godbless Lema jijini Arusha amekuwa akikubaliwa na hivi karibuni aliomba kibali cha mikutano afanye kwa siku saba alivyofanya siku tatu alivyoona hakuna watu aliacha kufanya, kwa sababu shida nyingi za wananchi zinatatuliwa na serikali”

RC Gambo asema Lema na meya sasa wamekubali kazi ya JPM - MwananchiAmesema katika utawala huu wapinzani wanapaswa kujipanga kwakuwa mambo mengi ambayo walikuwa wakiyapigia chapuo tayari Serikali ya Chama tawala inayafanya.

“Huu ni utawala ambao Wapinzani wanatakiwa kusoma alama za nyakati, kwa sababu yale mambo yote ambayo wao walikuwa wakiyapigia kelele Rais anayafanya”


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...