Search This Blog

Wednesday, March 4, 2020

Dar - Dodoma nauli zapanda

Wakati Waziri wa Ujenzi, Isack Kamwelwe akiahidi daraja la Kiyegeya barabara ya Morogoro-Dodoma lililosombwa na maji kuanza kutumika kuanzia saa 4:00 usiku wa kuamkia leo, nauli za mabasi zimepanda.

Nauli zilizopanda ni Dar es Salaam kwenda Dodoma kupitia njia ya Iringa.

Daraja hilo lililopo Gairo linalounganisha mikoa ya Dodoma na Morogoro lililosombwa na maji juzi saa 9:00 alasiri kufuatia mvu zinazoendelea.

Juzi kabla ya Serikali kufunga barabara hiyo mamia ya abiria na magari yalikwama eneo hilo huku baadhi wakilazimika kutumia njia mbadala.

Uchunguzi wa Mwananchi umebaini nauli kutoka Dar kwenda Dodoma kupitia Iringa ilikuwa Sh40,000 kutoka Sh22000 kwa basi daraja la kawaida; Sh28,000 hadi Sh45,000 daraja la kati; na Sh50,000 kutoka Sh35,000 daraja la maalumu (VIP) kupitia njia ya Iringa.

Umbali wa kutoka Dar-Iringa hadi Dodoma ni takriban kilomita 760, huku Dar-Moro hadi Dodoma ni kilomita 454.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...