China hii leo imeripoti kesi mpya 16 za virusi vya corona, ikiwa ni kiwango cha juu katika kipindi cha wiki moja.
Tume ya taifa ya afya imesema maambukizi hayo yanawahusisha watu wanaowasili kutokea nchi za nje na yameripotiwa kwenye majimbo matano yakiwemo Beijing na Shanghai.
Kesi nyingine nne za maambukizi zimeripotiwa Wuhan mji mkuu wa jimbo la Hubei, ambako virusi hivyo vilianzia. Idadi ya watu waliofariki China kutokana na maradhi hayo imefikia watu 3,199 huku zaidi ya 80,000 elfu wakiambukizwa.
Jimbo la Hubei lilikuwa limefungwa mwezi Januari na kuwaweka karantini wakaazi karibu milioni 56, lakini idadi ya kesi mpya za maambukizi imepungua katika wiki za hivi karibuni.
Mamlaka za mji huo sasa zimeanza kulegeza baadhi ya hatua zilizokuwa zikiwazuia watu kutoka nje ya makaazi yao, ingawa hakuna dalili za watu kuondoka ndani ya jimbo hilo.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment