Mkuu wa Shirika la Afya Duniani Afrika Dr. Matshidiso Moeti amewaambia waandishi habari kwamba bara hilo linashuhudia mabadiliko makubwa katika kuongezeka kwa maambukizi ya virusi vya corona.
Mataifa thelathini na sita kati ya 54 hadi sasa yamesharipoti maambukizi ya virusi hivyo ambayo jumla yake ni 720.
Hapo jana Chad na Niger zilitangaza kuthibitisha maambukizi yake ya kwanza.
Na kisa cha kwanza cha maambukizi ya virusi vya corona kikiwa kimeripotiwa wiki tatu zilizopita katika mataifa yaliyo kusini mwa jangwa la Sahara.
Mataifa mengine zaidi barani humo yametangaza kufunga mipaka yake kuzuia kusambaa kwa virusi hivyo katika bara lenye idadi ya watu wapatao bilioni 1.3.
Moeti amesema haamini kwamba idadi kubwa ya walioambukizwa barani humo wameshindwa kutambuliwa lakini amekubali kwamba kuna upungufu wa vifaa vya kufanyia vipimo vya virusi hivyo vya corona.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment