UONGOZI wa Yanga umesema kuwa mchezo wa kesho dhidi ya Tanzania Prisons hautakuwa mwepesi kutokana na ugumu wa timu ambayo watakutana nayo.
Prisons itashuka Uwanja wa Taifa kumenyana na Yanga, Februari 15, majira ya saa 1:00 usiku ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mechi zote mbili msimu huu ilipokutana na Yanga.
Mechi ya kwanza ya ligi ilichezwa Uwanja wa Samora na Prisons ilifungwa bao 1-0 lilifungwa na Patrick Sibomana na mechi ya pili ya Kombe la Shirikisho ilipigwa Uwanja wa Taifa ilikubali kichapo cha mabao 2-0 yaliyofungwa na Ikpe pamoja na Morrison.
Luc Eymael, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa wanatambua uimara wa wapinzani wao jambo litakalofanya mchezo kuwa mgumu.
"Haitakuwa kazi rahisi na mchezo utakuwa mgumu ila kikubwa ni maandalizi ambayo tunayafanya na mpaka sasa tupo vizuri, mashabiki wajitokeze kwa wingi kutupa sapoti," amesema.
Yanga ipo nafasi ya tatu kwenye msimamo ikiwa na pointi 38, Prisons ipo nafasi ya 12 ikiwa na pointi 25.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment