Search This Blog

Wednesday, February 26, 2020

Wilder alitumia Dola 60,000 kutengeneza vazi lililomponza

LAS VEGAS, MAREKANI . BONDIA Deontay Wilder alitumia Dola 60,000 kutengeneza vazi ambalo alilivaa wakati akiingia kupambana na Tyson Fury katika pambano la uzito wa juu duniani ambalo alichapwa kwa TKO katika raundi ya saba.

Kinachostaajabisha, licha ya kutumia pesa ndefu kutengeneza vazi hilo, lakini Wilder analalamika kuwa uzito wake ulichangia kupigwa katika pambano hilo lililofanyika Jumapili asubuhi katika Ukumbi wa MGM Grand Arena, Las Vegas, Marekani.

Vazi hilo la jeusi lililokuwa na mambo mengi ambayo yalilenga kutengeneza hofu kwa Fury, lilibuniwa na wabunifu wawili Cosmo na Donato ambao walikunja Dola 60,000 kwa kazi hiyo.

Wakati, Walder akilalamikia kuponzwa na vazi hilo, Promota wa Anthony Joshua, Eddie Hearn na yule wa Fury, Frank Warren wamemshangaa bondia huyo kwa kuja na sababu za kitoto kujitetea baada ya kula kichapo.

Let's block ads! (Why?)

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...