Jeshi la polisi mkoani Kagera linamshikilia Dezber Kahwa mwenye umri wa miaka 49 mkazi wa kijiji Kibengwe, Bukoba Vijijini kwa tuhuma za kusababisha kifo cha Alinda Leverian mwenye umri wa miaka 14.
Aliyeuawa ni mwanafunzi wa darasa la sita Shule ya Msingi Kilima, ambapo mtuhumiwa huyo alimtoa mimba kwa njia isiyokuwa halali na salama.
Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Revocatus Malimi amesema kuwa tukio hilo lilitokea Februari 08 mwaka huu nyumbani kwa Vedastina Cleophace, huku Kahwa ambaye alikuwa muuguzi katika zahanati ya Buza kabla ya kufukuzwa kazi na serikali wakati wa kuwaondoa watumishi hewa, kujaribu kumtoa mimba mwanafunzi huyo.
Mwili wa mwanafunzi huyo umefanyiwa uchunguzi na daktari wa binadamu katika hospitali ya Rufaa Bukoba na kubaini kuwa chanzo cha kifo hicho ni kutobolewa kwa mfuko wa uzazi na kuingizwa sumu.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment