Na Ahmad Mmow, Lindi
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Lindi Riziki Lulida amekabidhi msaada wa chakula tani 4 , vyandarua 500 na maturubai 200 kwa waathirika wa mafuriko katika vijiji vya Nanjima A , na Nanjima B jimbo la mchinga mkoani Lindi.
Akizungumza na Wananchi wa viijiji hivyo wakati akikabidhi misaada hiyo, alisema ameguswa na madhara mafuriko ambayo licha ya kusababisha watu wakose makazi, lakini pia yamepoteza uhai wa watu na mali zao. Kwahiyo ameona umuhimu wa kutoa misaada ili kuwasaidia waathirika waliopoteza ndugu na mali zao wakati wa mafuriko.
Alisema ametoa msaada huo kwa jamii iliyokumbwa na maafa baada ya kutembelea baadhi ya maeneo ya waathirika waliokumbwa na mafuriko Lindi vijijini .ikiwemo Kitomanga na Nangaru.
“Mimi mbunge wenu wa viti maalumu nimetoa msaada wa chakula, marutubai na vyandarua kwa sasa lakini wakati bado nitaendelea kuwaunga mkono serikali, nitahakikisha tunaendelea kushirikiana katika wakati huu wa shida na wakati wa raha na nyakati zote. Tupo pamoja, nitawahudumia," alisema Lulida.
Mbunge huyo alisema juhudi za makusudi zinahitajika katika kipindi hiki kigumu kutokana na waathirika kuhitaji misaada ya kijamii baada ya kukumbwa na hayo yaliyosababisha wapoteze makazi ,vyakula , mifugo na mazao yao.
Mmoja wa athirika hao, Baraza Maduhu mkazi wa kijiji cha Kitomanga akizungumza kwanianiaba ya wanakijiji wenzake licha ya kumshukuru mbunge huyo na serikali kwa kutoa misaada mbalimbali alisema wanatunaimani itawasaidia na kujipanga upya kuendesha familia zao.
.
Lakini pia, Maduhu aliiomba serikali iwapatie maneo mengine ili waache kuishi mabondeni. Ambapo mvua kubwa ikinyesha maji hujaa mtoni na kuingia ndani kusababisha mafuriko.
Kwaupande wake mkuu wa wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga alisema mbunge huyo ameonesha moyo wa kuthamini jamii yenye matatizo kwa kujali janga la mafuriko ambalo limeathiri kwa kiasi kikubwa shughuli za maendeleo. Huku akiwaomba wadau wengine kuiga mfano huo.
Alisema kunahitaji sana misaada,kama ya chakula, nguo na dawa. Kwani mpaka sasa kuna kambi nne zenye watu zaidi 843 waliokumbwa na mafuriko Lindi vijijini.
Alisema serikali imetenga maeneo ya viwanja ambavyo vitagawiwa kwa wananchi wote waliokumbwa na mafuriko ili wakaendelee na shughuli zao za kiuchumi na maendeleo.

No comments:
Post a Comment