Search This Blog

Monday, February 24, 2020

Mastaa wafulika siku ya kuwakumbuka na kusherekea maisha ya Kobe Bryant na mwanaye


Marekani Kwenye ukumbi maarufu wa Staples Center uliopo mjini Los Angeles ambao unaingiza watu 20,000, imefanyika shughuli  ya kuwakumbuka na kusherekea maisha ya marehemu Kobe Bryant na binti yake Gianna.

Katika shughuli hiyo wamehudhuria watu maarufu mbali mbali wakiwemo mastaa wa muziki, movie na hata wachezaji wa mchezo wa Basketball ambao wamefika katika ukumbi huo uliowahi kutumika kuwaaaga baadhi ya watu maarufu waliotangulia mbele za haki kama Michael Jackson, Nipsey Hussle na wengine.

Kama utakumbuka Kobe Bryant na mwanae Gianna walizikwa February 7, 2019 kwa Siri, mazishi yalihudhuriwa na ndugu na jamaa wakaribu kisha wakaitenga siku ya leo kwaajili ya watu wengine kuwa kumbuka na kusherekea maisha ya Marehemu hao na Msanii aliyefungua kwa performance ni msanii Beyonce.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...