Rais wa Manzese Madee Seneda, amemshauri mpenzi mpya wa Dogo Janja "Quenlinnah" kwa kumwambia ategemee mengi kwa sababu yupo kwenye mahusiano na mtu maarufu.
Madee amesema hayo baada ya Dogo Janja kumvalisha pete ya uchumba mpenzi wake huyo siku ya jana Februari 10, 2020, kwenye boti wakati wanarudi Dar es Salaam wakitokea visiwani Zanzibar.
"Mpenzi wa Dogo Janja ajue kabisa yupo kwenye mahusiano na mtu maarufu na yeye anaelekea kuwa maarufu muda sio mrefu, kwahiyo asisikilize maneno ya watu na ategemee mengi ambayo yatatikisa mahusiano yao ambayo ni mapya" amesema Madee.
Aidha katika msimu huu wa wapendanao Dogo Janja mwenyewe amesema "Msimu wa mapenzi umekuwa mzuri kwetu kwani nimeufurahia sana mimi na mpenzi wangu kule visiwani Zanzibar, nikiwa na familia yangu kama Linah, Recho na Madee".
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment