SERIKALI imesema itaendelea kushirikiana na wafanyabiashara, wawekezaji na wadau wote wa maendeleo ambao wanawekeza nchini ikiwa ni pamoja na kuweka mazingira rafiki kwao.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe Anthony Mavunde,alipokuwa akizundua pamoja na uwekaji wa jiwe la msingi katika kituo cha mafuta cha Amire Oil inayofanya biashara ya mafuta mikoa mbalimbali nchini.
Mhe Mavunde amesema serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk John Magufuli inathamini wawekezaji kutokana na mchango wao katika kutoa ajira na kukuza pato la Taifa kupitia kodi wanazolipa.
” Niupongeze uongozi wa Kampuni hii kwa kukuona umuhimu na ulazima wa kuja kuwekeza katika Jiji la Dodoma kwani kufanya hivyo kutaongeza fursa kubwa za ajira kwa vijana ikizingatiwa tayari mmeshaajiri ajira 20 mpaka sasa kwa wananchi wa Dodoma.
Sisi kama Serikali tunaendelea kutoa wito kwa wawekezaji wengine kuja kuwekeza katika Jiji hili ambalo ndio Makao Makuu ya Serikali lakini pia kuna maeneo mengi ya Uwekezaji na rafiki kwa ajili ya kujenga viwanda, hoteli na hata majengo ya kibiashara, ” Amesema Mhe Mavunde.
Awali Msemaji wa makampuni ya Admire Oil Bw.Mohamed Ibrahim ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji jambo ambalo linaongeza ari kwao ya kuzidi kufanya Uwekezaji katika maeneo mengi zaidi nchini.
” Kwa kweli serikali ya Rais Magufuli imetoa mazingira rafiki sana kwa wafanyabiashara hasa wazalendo. Sisi tunaahidi kuendelea kushirikiana na serikali yetu ili kufikia ndoto ya Rais wetu ya Tanzania ya viwanda.
Tunafahamu lengo la kila mfanyabiashara ni kuwekeza na kupata faida lakini kampuni yetu ya Admire moja kati ya malengo yake makubwa ni kugawa ajira kwa akina Mama na vijana wengi nchini, ” Amesema Ibrahim.
Aidha amesema kuwa wameajiri vijana wengi sana takribani watu mia moja na hamsini nchini na kati ya hao wengi wao ni wanawake ili tu kuwainua pamoja na kuwawezesha kiuchumi.
Kampuni ya admire Oil ina matawi mengi katika mikoa mbalimbali nchi kituo kikubwa kikiwa ni mkoa wa Pwani pamoja na mikoa ya Mwanza,Arusha,Mbeya,Dar es Salaam na Dodoma tunapatikana katika huduma ya mafuta.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment