Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewaonya vikali mashabiki wa timu za Simba na Yanga kwa kuwataka kuwa wastaarabu wakati wote wa mchezo huo kuelekea pambano la watani wa jadi linalotarajiwa kufanyika Jumamosi wiki hii,
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, alisema wamejipanga kikamilifu kuimarisha ulinzi katika mchezo huo, akiwataka mashabiki wote watakaofika kutazama mchezo huyo kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani.
Alisema pamoja na mapenzi yao kwa timu hizo, mashabiki hao wanatakiwa kushabikia mchezo huo kwa ustaraabu bila kurushiana chupa na kuharibu miundombinu ya uwanja na mambo mengine jambo litakaoufanya mchezo huo kumalizika kwa amani.
“Hatutasita kuwachukulia hatua kali watu wote watakaofanya mambo yasiyo ya kistaarabu siku ya mchezo huo, tutakuwa tumejipanga na kujiimarisha katika maeneo yote ya uwanja ili kuhakikisha mchezo unamalizika bila kuwapo na vurugu kutoka kwa mashabiki,” alisema Mambosasa.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment