Search This Blog

Wednesday, January 1, 2020

Jeshi la polisi lawaonya washabiki wa Simba na Yanga

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewaonya vikali  mashabiki wa timu za Simba na Yanga kwa kuwataka kuwa wastaarabu wakati wote wa mchezo huo kuelekea pambano la watani wa jadi linalotarajiwa kufanyika Jumamosi wiki hii,

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, alisema wamejipanga kikamilifu kuimarisha ulinzi katika mchezo huo, akiwataka mashabiki wote watakaofika kutazama mchezo huyo kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani.

Alisema pamoja na mapenzi yao kwa timu hizo, mashabiki hao wanatakiwa kushabikia mchezo huo kwa ustaraabu bila kurushiana chupa na kuharibu miundombinu ya uwanja na mambo mengine jambo litakaoufanya mchezo huo kumalizika kwa amani.

“Hatutasita kuwachukulia hatua kali watu wote watakaofanya mambo yasiyo ya kistaarabu siku ya mchezo huo, tutakuwa tumejipanga na kujiimarisha katika maeneo yote ya uwanja ili kuhakikisha mchezo unamalizika bila kuwapo na vurugu kutoka kwa mashabiki,” alisema Mambosasa.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...