Search This Blog
Monday, January 27, 2020
Waziri Kabudi: Hakuna Mtanzania aliyekumbwa na maambukizi ya ugonjwa wa Corona
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi, amesema kuwa hakuna Mtanzania yeyote anayeishi nchini China, aliyekumbwa na maambukizi ya virusi vya homa ya Corona, vilivyozuka katika Mataifa ya Marekani, China, Thailand, Korea Kusini na Japan.
Waziri Kabudi ameyasema hayo wakati akitoa ufafanuzi juu ya hali ya Watanzania waishio nchini China na kusema kuwa Tanzania ina wanafunzi takribani 4000, ambapo katika mji wa Wuhan kuna wanafunzi 400 na kwamba kwa mujibu wa Balozi wa Tanzania Nchini China, Balozi Mbelwa Kairuki, ameihakikishia Serikali kuwa mpaka sasa hakuna mtanzania yeyote aliyeathiriwa ama kukumbwa na maradhi hayo.
Ameongeza kuwa Tanzania inaendelea kufuatilia kwa ukaribu kujua maendeleo na hali za Watanzania wanaoishi jimboni Wuhan na China kwa ujumla na kuwataka Watanzania kuwa makini na suala la kutoa taarifa zisizo rasmi ama uvumi, kwani kwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za Tanzania na kuwataka kuwa na subira ili kupata taarifa rasmi kutoka serikalini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment