Search This Blog
Monday, January 20, 2020
Waasi Watumia Ndege zisizo na Rubani Kushambulia Wanajeshi Yemen
Zaidi ya wanajeshi 80 wa Yemen wameuwawa na wengine wengi wamejeruhiwa kwenye Shambulizi la Kombora la Ndege zisizokuwa na Rubani lililofanywa na Waasi wa Houthi katikati ya Yemen.
Mashambulizi hayo yanafuatia miezi kadhaa ya utulivu kiasi katika Nchi hiyo inayokabiliwa na vita kati ya Waasi wa Kihouthi wanaoungwa mkono na Iran.
Waasi wa kihouthi walishambulia msikiti mmoja katika Kambi ya Kijeshi iliyoko kwenye mkoa wa kati wa Marib kilomita 170 Mashariki mwa Mji mkuu Sanaa wakati wa sala ya Magharibi.
Mashambulizi yamefanyika siku moja baada ya wanajeshi wa Serikali wanaoungwa mkono na Kikosi cha Muungano kuanzisha operesheni kubwa dhidi ya Wahouthi katika mkoa wa Nihm Kaskazini mwa Sanaa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment