Search This Blog

Tuesday, January 7, 2020

TPRI,TOSC waagizwa kuzunguka nchi nzima kukagua usahihi wa mbegu

Na Amiri kilagalila-Njombe



Waziri wa kilimo nchini Japhet Hasunga ameziagiza taasisi ya kudhibiti ubora wa Mbegu (TOSC) na taasisi ya utafiti wa viuatilifu vya kudhibiti visumbufu katika ukanda wa Kitropiki (TPRI),kuhakikisha wanazunguka kwenye mabohari na mawakala nchi nzima kuona usahihi wa madawa na mbegu zinazotumika.

Waziri hasunga ametoa agizo hilo mkoani Njombe wakati akikagua uwepo wa pembejeo kwa wauzaji wa pembejeo mjini Makambako.

“Laikini taasisi ya TPRI pamoja TOSC nitumie fursa hii kuwaagiza wazunguke katika maeneo mbalimbali kwenye bohari kwa mawakala nchi nzima,wakague waone usahihi wa mbegu lakini waone usahihi wa madawa yanayotumika yote,na wale ambao itaonekana wamevunja taratibu na sheria za nchi yaani wameleta vitu feki basi hatua kali zichukuliwe kwa mujibu wa sheria na waadhibiwe kwa kadri itakavyowezekana”alisema Japhet Hasunga

Katika hatua nyingine amemuagiza TBA kumsimamia mkandarasi wa ujenzi wa maghala ya kuhifadhia mahindi yanayojengwa mjini Makambako kuhakikisha mradi huo hadi kufikia 30-6-2020 uwe umekamilika na kuanza kutumika.

“Kufikia tarehe 30 June mhakikishe wanakamilisha wakabidhi ili Julai tuanze kutumia hivi vihenge hatutakuwa na sababu zingine zozote za kuongeza muda,na kwasababu huu mradi ulitakiwa uwe umekamilika disemba kumekuwa na changamoto za hapa na pale sasa tumepeleka June,nah ii itatusaidia sasa tuanze kupambana na sumu kuvu”alisema Japhet Hasunga

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...