SVEN Vanderbroek, Kocha Mkuu wa Simba leo ana kazi mbele ya Mbao FC kwenye mchezo utakaochezwa Uwanja wa CCM Kirumba.
Sven anaingia kibaruani akiwa na kumbukumbu ya kupokea kichapo cha bao 1-0 mbele ya Mtibwa Sugar kwenye fainali ya Kombe la Mapinduzi na kulipoteza kombe la kwanza.
Leo Simba itamenyana na Mbao FC majira ya saa 10:00 jioni na kazi kubwa itakuwa kulipa kisasi cha msimu uliopita baada ya kufungwa bao 1-0 msimu uliopita mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa CCM Kirumba.
Bao pekee lilifungwa na Said Khamis, Jr kwa mkwaju wa penalti na ilisababisha aliyekuwa Kocha Mkuu wa wakati huo, Patrick Aussems, kutupiwa chupa na mashabiki kwenye mchezo wake wa nne ambao alipoteza.
Beki kisiki wa Simba, Pascal Wawa amesema maandalizi yanaendelea kila siku na wanahitaji kuona wanapata matokeo.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...

No comments:
Post a Comment