Search This Blog
Friday, January 24, 2020
Serikali: Hakuna virusi vya Corona Tanzania
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto imetoa tahadhari ya mlipuko wa Virusi vya Corona na kusema wamekuwa wakifuatilia mlipuko huo tangu ulipoanza Nchini China na kusambaa katika mataifa mengine.
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya imesema, hakuna muathirika wa Virusi vya Corona nchini Tanzania. Hata hivyo imeweka wazi kuwa, kutokana na Mahusiano ya Kijamii na Kibiashara yaliyopo kati ya Tanzania na Bara la Asia, kuna hatari kuwa Virusi hivyo vinaweza kuingia nchini.
Magufuli aruhusu makontena ya Makinikia yaliyozuiwa 2017 yauzwe
Serikali imetoa tahadhari wa Watanzania wanaosafiri kuelekea China, pamoja na Thailand, Japan, Marekani na Korea Kusini ambazo zimeripoti maambukizi hayo. Tahadhari pia imetolewa kwa wanaopokea wageni kutoka nchi hizo.
Tayari watu 830 wameshaambukizwa kirusi hicho, huku 26 wakipoteza maisha na mamilioni wengine wamewekwa chini ya karantini katika juhudi za kujaribu kudhibiti kusambaa kwake.
Hukumu yatolewa kwa watanzania waliozamia Afrika kusini
Taasisi inayoshughulikia chanjo na kinga za maradhi duniani imesema, chanjo dhidi ya kirusi hicho inaweza kupatikana katika kipindi cha mwaka mmoja unaokuja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment