Search This Blog

Thursday, January 9, 2020

Mwalimu auwawa kisa matokeo mabaya

Watu wawili wamekamatwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumshambulia na mapanga mwalimu wa shule ya msingi hadi kumsababishia kifo.

Washukiwa wawili ambao ni wazazi wawili  wanazuiliwa huku uchunguzi ukifanywa dhidi yao

Wambua Mwangangi na Chris Kyalo Muli wanasemekana kumuua mwalimu huyo baada ya shule yake kutoa matokeo mabaya katika mtihani wa kitaifa wa KCPE mwaka wa 2019.

Daisy Mbathe aliripotiwa kushambuliwa kwa panga kabla ya mwili wake kuteketezwa na washukiwa hao.

Mbathe ambaye aliuawa Januari 6, 2020 alikuwa mwalimu katika shule ya msingi ya Ndooni.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...