Takriban watu 14 wengi wakiwa wanafunzi wamekufa baada ya basi walililokuwa wakisafiria kukanyaga bomu kaskazini magharibi ya Burkina Fasso wakiwa njiani kurejea shuleni baada ya mapumziko ya mwisho wa mwaka.
Kulingana na msemaji wa mkoa wa Boucle du Mouhoun kulikotokea kisa hicho amesema watu wengine wanne wamejeruhiwa kutokana mlipuko huko.
Hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulizi hilo lakini makundi ya itikadi kali yenye mafungano na Al -Qaeda pamoja na kundi linalojiita Dola la Kiislamu yamekuwa yakilaumiwa kwa matukio kama hayo nchini Burkina Fas.
Vifo hivyo vimetokea ikiwa ni wiki moja baada ya watu 35 wengi wakiwa wanawake kuuwawa kwenye shambulizi lililotokea kwenye mji wa kaskazini wa Arbinda huku wanajeshi saba waliuwawa kwenye shambulizi tofauti katika kambi ya jeshi karibu na eneo hilo.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment