Search This Blog

Tuesday, January 7, 2020

Baada ya kufungiwa Dudubaya apanga kuwaburuza mahakamani Basata

Msanii wa bongo fleva Godfrey Tumaini maarufu kama Dudubaya amewajibu tena basata na kusema kuwa hajapokea barua yoyote ya kufungiwa kufanya sanaa na amehaidi kuwapeleka mahakamani Basata.

Dudu baya amesema atowaomba msama Basata na hata akipata show yoyote ataendelea kuifanya kwakuwa atajapewa barua yoyote.

"Sijapokea barua yoyote ya kufungiwa kufanya kazi ya sanaa kwahiyo hata kesho nikipata show ntafanya kama kawaida na nikishapokea hiyo barua ntakaa na mwanasheria wangu na nikishajua wameandika nini lazima niwatie mahakamani'' alisema Dudubaya

Ameendelea kusema kuwa anaiamini serikali ya awamu ya tano ya Rais Magufuli ni ya ukweli, uwazi na haki anaamini atashinda kesi.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...