Search This Blog
Monday, December 30, 2019
Yanga Waitumia Salamu SIMBA...Yaibamiza Biashara United
Klabu ya Yanga imeibuka kidedea baada ya kuitandika Biashara United bao 1-0 kwenye mchezo wa ligi kuu uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa.
Bao pekee la ushindi kwa Yanga limefungwa na Tariq Seif dakika ya 84 akimalizia pasi ya nahodha Papy Tshishimbi akiwa ndani ya 18 na kuzamisha moja kwa moja wavuni.
Seif ambaye aliwahi kucheza Biashara United kabla ya kusajiliwa hivi karibuni kwenye dirisha dogo ndani ya Yanga akitokea nchini Misri amesema kuwa anaona fahari kuipa pointi tatu, timu yake.
"Nimefurahi kuona nimeipa ushindi timu yangu inaamanisha kwamba ninaweza na nitaendelea kupambana kwa kushirikiana na wenzangu ili kuwa bora zaidi," amesema.
Yangaimecheza jumla ya mechi 11 inafikisha jumla ya pointi 24 sawa na Kagera Sugar inakuwa nafasi ya pili kwa tofauti ya mabao ya kufungwa ikiwa nyuma ya Simba walio kileleni wenye pointi 31 wakiwa wamecheza jumla ya mechi 12.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment