Search This Blog
Monday, December 30, 2019
Wanafunzi 17,820 kupangishwa nyumba za NSSF Mtoni Kijichi Dar
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limesaini makubaliano ya awali na vyuo vya elimu ya juu vilivyopo Dar es Salaam, kwa ajili ya kuwapangisha wanafunzi nyumba zilizopo Mtoni Kijichi.
Akizungumza mara baada ya kuweka saini makubaliano hayo Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, William Erio, alisema zaidi ya wanafunzi 17,820, watanufaika na nyumba hizo katika awamu ya kwanza kutoka Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo cha Teknolojia cha Dar es Salaam (DIT), Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.
Aidha aliwataka Watanzania kuchangamkia fursa ya kukopa nyumba zilizopo Toangoma na Dungu, ambazo zinafaa kwa makazi, kwa kupangishwa ama kwa kuuza.
Vile Vile, alisema uwepo wa nyumba hizi ni fursa kwa taasisi za fedha kuanza utaratibu kwa wanaotaka kupanga au kununua nyumba hizo waanze utaratibu wa kuwakopesha na ikiwezekana kwa riba maalumu ambayo itakuwa nafuu.
Alisema ni ruksa kwa Watanzania wote kununua nyumba hizo kwani ni nyingi na za aina tofauti zipo za vyumba vitatu mpaka vitano.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment