Search This Blog

Sunday, December 15, 2019

Serikali yabainisha fursa ya ufugaji samaki ukanda wa Pwani


Serikali imesema inahakikisha sera yake ya kuhamasisha wananchi kufuga samaki inatekelezwa kote nchini ili kutosheleza mahitaji ya soko la samaki nchini pamoja na kukuza pato la taifa na mtu mmoja mmoja.

Akizungumza Mjini Mtwara, wakati akifungua tawi la Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Kampasi ya Mikindani Mkoani Mtwara, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega ameiagiza FETA kwa kushirikiana na Idara ya Ukuzaji Viumbe kwenye Maji kutoka katika wizara hiyo, kuandaa mitaala ya ufugaji viumbe kwenye maji wakiwemo samaki, kaa, majongoo bahari na Kambakochi kwa ajili ya wananchi wa Ukanda wa Pwani ili waweze kuongeza vipato vyao kupitia fursa ya ufugaji.

Aidha Ulega ameagiza uundwaji wa vikundi vya uzalishaji kaa, Kambakochi, majongoo bahari pamoja na wazalishaji wa zao la mwani ili iwe rahisi kwa vikundi hivyo kutambulika rasmi pindi mazao yao yanapohitajika sokoni, na watu waweze kufika katika mashamba yao ya ufugaji kwa ajili ya kuvua samaki na viumbe vingine wakiwemo kaa, kambakochi na majongoo bahari ambao wamekuwa na soko kubwa sana na mahitaji yake kuongezeka katika baadhi ya maeneo zikiwemo hoteli za kitalii.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mafunzo kutoka FETA, Ambakisye Simtoe amesema chuo hicho kimepanga kuzalisha wagani kwa ajili ya kuendeleza na kukuza tasnia ya uvuvi nchini pamoja na kununua mashine ya kuzalisha vifaranga bora ili iwe rahisi kwa wananchi wa Ukanda wa Pwani kupata vifaranga hivyo kwa bei nafuu huku katika risala ya wanafunzi hao wakisema mafunzo waliyoyapata yakiwemo ya ufugaji wa samaki yatawawezesha kujiajiri.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...