Search This Blog

Sunday, December 29, 2019

Mwili wa Faru Fausta kuhifadhiwa


Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamis Kigwangala amesema serikali inakusudia kuukausha na kuutunza mwili wa faru Fausta kwenye jumba la makumbusho eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.

Faru Fausta amekufa akiwa na umri wa miaka 57 na inaaminika ndiye faru aliyekufa akiwa na umri mkubwa zaidi duniani.

“Tunakusudia kumkausha na kuutunza mwili wake kwenye Jumba la Makumbusho pale eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, aidha ninawapongeza sana wahifadhi wetu wa Ngorongoro kwa kazi nzuri ya kumtunza Faru Fausta, Faru wengine wengi na Hifadhi yote kwa ujumla” amesema Waziri Kigwangala.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...