Search This Blog
Tuesday, December 31, 2019
Mtandao wa SIMU wa MTN Washutumiwa Kufadhili Magaidi
Shutuma hizo zilizotolewa katika Mahakama ya nchini Marekani siku ya Ijumaa zinadai Mtandao huo mkubwa wa simu Afrika unafadhili kwa kutoa fedha kwa Makundi ya Kigaidi Nchini Afghanistan
Katika shutuma hizo ambapo Kampuni nyingine tano zimehusishwa inadaiwa kuwa MTN ilivunja sheria ya kukabiliana na ugaidi ya Marekani
MTN inadaiwa kutoa rushwa kwa Al-Qaeda na Taliban ili wasiweze kuwekeza pesa nyingi kwa ajili ya kulinda mitambo yao nchini humo ambapo fedha hizo zinadaiwa kutumika kwenye mashambulio kati ya mwaka 2009 hadi 2017
Pia, inasemekana fedha hizo zilizotolewa na mtandao huo wa mawasiliano unaoshika nafasi ya 8 kwa duniani kote, ukiwa na Watumiaji zaidi ya milioni 240, zimetumika kununua silaha hivyo kuvunja sheria ya kupambana na ugaidi
Mwaka 2015, Kampuni hiyo ililipishwa fidia ya Dola Bilioni 5 na Serikali ya Nigeria baada ya kushindwa kudhibiti laini za simu ambazo hazikusajiliwa, ambapo fidia hiyo baadaye ilipunguzwa hadi kufikia Dola Bilioni 1.7
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment