Search This Blog
Monday, December 30, 2019
Mchezaji wa Yanga atakayefanya vizuri mechi dhidi ya Simba kupewa zawadi nono na GSM
Kuelekea mechi ya watani wa jadi, Simba na Yanga itakayochezwa Jumamosi, Kampuni ya GSM Group, ambao ni moja ya wadhamini wa Yanga inatarajia kutoa zawadi ya godoro kwa mchezaji wa klabu hiyo atakayeibuka nyota wa mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari Meneja Masoko na Mawasiliano wa GSM Group, Matina Nkurlu, alisema wameamua kutoa zawadi hiyo ili kuwapa morari wachezaji wa Yanga.
Alisema wao kama wadhamini wa Yanga ni wajibu wao kuhakikisha timu hiyo inawapa raha mashabiki wake kwa kushinda mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka hapa nchini na Afrika Mashariki kwa ujumla.
"Kuelekea mechi ya kukata na shoka kati ya watani wa jadi, Simba na Yanga, moja ya wadhamini wakuu wa timu ya Yanga, GSM Group kupitia godoro chapa GSM, tutatoa zawadi nono kwa mchezaji bora wa timu ya Yanga wakati wa mechi Yanga na Simba kwa kumzawadia godoro la nchi 5x6x8," alisema.
Aliendelea kwa kusema, "Tunaamini zawadi hii itawaongezea wachezaji morali ya kupambana kuiwezesha Yanga kupata ushindi na hivyo kuwapa raha mashabiki wao na kuendelea kupata matokeo chanya kwa mechi zingine zijazo,".
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment