Search This Blog
Monday, December 9, 2019
Mbeya: Auawa Akituhumiwa Kuwatesa Wananchi Kwa Uchawi
Jeshi la Polisi linawashikilia Watu watatu wakidaiwa kumuua John Mwakarundwa(62), Mkazi wa Kijiji cha Nkunga Wilayani Rungwe tukio ambalo linahusishwa na imani za kishirikina
Kamanda wa Polisi Mbeya Ulrich Matei amesema, Mwakarunda alikuwa anatuhumiwa kununua uchawi Malawi hivyo Wananchi wa eneo hilo walikuwa na hasira nae wakidai anawatesa
Amesema, Watuhumiwa walimvamia Mwakarundwa na kumkatakata na vitu vyenye ncha kali maeneo ya kisogoni, taya la kushoto na tumboni
RPC amebainisha, "Watuhumiwa wanadai wamefanya hivyo ili kulipiza kisasi na baada ya kuuawa kwake Wananchi walikuwa wanashangilia wakifurahia kifo chake."
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment