Search This Blog

Tuesday, December 10, 2019

Kocha wa Napoli afutwa kazi baada ya kuichapa KRC Genk goli 4-0


Klabu ya soka ya Napoli ya Italy imemfukuza kazi aliyekuwa kocha wao Carlo Ancelotti saa machache baada ya kuiongoza timu hiyo kuingia hatua ya mtoano kwenye Champions League.

Ancelotti ambaye ameiongoza Napoli kwa miezi 19, kabla ya kushinda mechi ya jana 4 - 0 dhidi ya Genk ya Belgium, Napoli walikuwa wamecheza mechi tisa zilizopita bila ya kushinda kwenye mashindano yote.

Timu za Everton na Arsenal za Uingereza zinafanya jitihada za kumchukua Ancelotti kuwa kocha wao.

Mchezaji na Kocha wa zamani wa AC Milan Gennaro Gattuso anategemewa kuiongoza Napoli kwa mkataba wa miezi 6.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...